Wananchi wa
eneo la kwa morombo mkoani arusha wapo hatarini kupatwa na magonjwa ya milipuko
kutokana na uchafu wa mazingira katika maeneo hayo
Maeneo hayo
ya kwa morombo wananchi wamekuwa wakiishi katika mazingira machafu na hatarishi
uku wengine wakikiri kupatwa na magonjwa ya milipuko kama vile kipindupindu,
kichocho na kuhara damu
Melina
Lengidale ni moja wa mkaazi wa kata ya terati eneo la kwa morombo ambapo
amesema tatizo hili limekuwa la muda mrefu bila kufanyiwa ufumbuzi wa aina
yeyote
Aidha
ameeleza viongozi wanaoingia madarakani wamekuwa wakihaidi kutatua tatizo
hilo ama changamoto hizo hii ambayo
imekuwa kero kubwa kwa wanaanchi lakini waingiapo madarakani hushindwa kutimiza
ahadi zao
“viongozi
wote hii ni kama hawamu ya pili kila uongozi ukiingia madarakani wala hata
hawasimamii swala hili sio la maji wala barabara wote wanatuacha njia panda”
| Kulia mmoja wa wafanya biashara katika eneo hilo la kwa morombo Bi Florida ngonyani akifanya maojiano na mwandishi wetu Janeth Sisso jana (picha na Charles Chami) |
Hata hivyo viongozi
wa eneo hilo la kwa morombo akiwemo mwenyekiti wa kijiji hicho bwana Frances
Mbise amekiri kuwepo na tatizo hilo na kuhaidi kulifanyia kazi tatizo hilo Habari na Janeth sisso
No comments:
Post a Comment