Fundi mitando bw.Aziz Mwinuka akitoa ufafanuzi juu ya mambo yanayoikabili studio za Ajtc Radio huku mwandishi wa Ajtc Bi.Lilian Deus( Picha na Nurdin Pallangyo)
Na.LILIAN DEUS.
Wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari na utangazaji
Arusha (AJTC) wameaswa kutumi muda wao kufanya mazoezi kwa vitendo ya uandishi
wa habari na kutangaza na kuandaa vipindi tofauti vya Radio ili wawaze kujijenga
na kuwa wazuri katika tansia hii ya uandishi.
Rai hiyo imetokewa na mmoja wa viongozi wa studio katika
chuo hicho ambaye pia ni fundi mitambo mkuu wa Radio AJTC Bw.Aziz Mwinuka
wakati akizungumza na mwandishi wa Ajtc
Radio.
Amesema wanafunzi wengi wamekuwa wavivu katika suala zima la
kutangaza na kuandaa vipindi vya Radio jambo ambalo limekuwa kama ni mazoea yao
Pia bw.Mwinuka amesema kuwa studio yao inakabiliwa na uhaba
wa vifaa vya kisasa( digitali) kama vile vipaza sauti yaani microphones na
Mixer lakini kutokuwa na uwepo wa vifaa hivyo hakukwamishi shughuli za studio.
No comments:
Post a Comment