Tuesday, 12 August 2014

MAZINGIRA MACHAFU KERO KWA WAKAZI WA OLASIT.



















Twaha Yahaya mkazi wa Olasit akitupa taka katika eneo la barabara iliyopo karibu na makazi ya watu.(Picha na Grace Mboya.)


NA;
       Grace Mboya,
             ARUSHA.


 Wananchi wa kata ya olasiti iliyopo Mkoani Arusha wameulalamikia uongozi wa vijiji vyake kwa kutokuweka utaratibu mzuri wa utunzaji wa mazingira.


         Malalamiko hayo yametolewa hivi karibuni na baadhi ya wakazi wa eneo hilo baada ya kufanya mazungumzo na mwandishi wetu kuhusiana na kuzagaa kwa uchafu unaonekana kuwa kero bembezoni mwa barabara za kata hiyo.
 















 Hali ya mazingira ya kijiji cha Olast inavyoonekana kuwa atarishi kwa afya za wananchi wa eneo hilo.(Picha na Grace Mboya)

 Walisema kuwa awali walikuwa na utaratibu wa kuzikusanya taka hizo bembezoni mwa barabara katika maeneo yaliyotengwa kwa siku tofautitofauti kulingana na mgao  wa vijiji na gari linafika kwa siku hiyohiyo kuzibeba na kuzipeleka katika jalala kuu la manispaa.
           “Yaani mwanzoni tulikuwa na utaratibu mzuri wa kuzikusanya hizi takataka na huwezi kuona hali chafu kama unayoiona ila kwa sasa atuelewi maana gari tuna muda sana atujaliona”.Alisema Hadija Yahaya mkazi wa eneo hilo.
            Pia walieleza hofu yao kuhusiana na magonjwa ya mlipuko yanayoweza kusababishwa na mazingira hayo yasiyo rafiki kwa afya zao kwani vituo hivyo vipo jirani na makazi ya watu na kuomba uongozi  kuweka utaratibu mpya kama huo wa awali umeshindikana.
       












Mwandishi wetu Grace Mboya akifanya mazungumzo na Elia Kambai mkazi wa Olasiti kuhusiana na hali ya mazingira katika kijiji hicho.(Picha na mpiga picha wetu.)
  Kwa upande wa baadhi ya wapangaji wa kata hiyo walisema kwao hiyo ni fursa kwani watazichoma taka hizo ili kuepuka kutozwa kiwango cha juu cha fedha ambacho wanatozwa kwa sasa.
    
 “Tulikubaliana kuwa sisi wapangaji tunatakiwa kulipa elfu moja na wenye nyumba za familia wanalipa elfu tatu pamoja na wenye vituo vya biashara lakini kwa sasa wapangaji tunaambiwa tulipe elfu moja mia tano heri tu hilo gari lisije tutazichoma wenyewe”.alieleza John Peter mpangaji wa eneo hilo.
        Juhudi za kumtafuta kiongozi wa kijiji cha olasiti hazikuzaa matunda baada ya kufika katika ofisi yake na kukuta imefungwa na kutokupatikana kwenye namba yake ya simu.

  


   






No comments:

Post a Comment