Mkufuzi wa chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha Adson Kagiye akihojiwa na mwandishi wa AJTC Radio Jesca Willy kuhusu wanafunzi wanaohama Hostel na kwenda kupanga vyumba.(Picha na Johaness Johnson)
HABARI NA JESCA WILLY
Wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari na
utangazaji Arusha, wanaoishi
nje ya hostel, wameshauriwa kufuata
sheria za nchi, nakufuata kilicho
weleta chuoni hapo ili kutimiza
malengo waliyo jiwekea
katika katika maisha yao.
Kauli hiyo
imetolewa na Mkufunzi wa chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha, Bw.Adison Kagiye, alipokuwa anahojiwa na Ajtc
redio nje ya ofisi yake hapo jana .
Bw.Adison
Kagiye amesema kuwa, chanzo cha kuhama kwa wanafunzi hao ni kutokana na kukosa
uhuru, kusikiliza maneno ya watu, na kushindwa kulipa gharama za hostel, hivyo kupelekea
kuhama ili kuepuka matatizo hayo yanayo
wakabili.
Mkufunzi
huyo mefafanua zaidi kwakusema kuwa,
wanafunzi wana maamuzi yakuchagua sehemu wanayo taka kuishi wao wenyewe, bila kupangiwa na mtu yeyote
,kwani nao ni raia kama wengine wanao
ishi kwa kujitegemea
Bw. Adsoni
ameongeza kwakusema, zipo changamoto mbalimbali zinazo wakabili kwa kuama kwa
wanafunzi, mojawapo ikiwa ni kukosa fedha, wengine kutoweza kumaliza fedha wanazo
daiwa pia hata kuchomwa visu kwa wanafunzi wanao ishi nje ya hostel ni moja ya
changamoto wanazokumbana nazo.
Mkufunzi
huyo bw. Adson kagiye amemalizia kwa kusema kuwa, wanafunzi wote wanaokaa nje
na ndani ya hostel ,wanatakiwa wasome ili kuepuka kufeli katika masomo yao,
kwani kufeli kunachangiwa na wote wanao kaa nje na ndani ya hostel.
No comments:
Post a Comment