Wednesday, 13 August 2014

HABARI KIMATAIFA : Mtuhumiwa azua kihoja mahakamani Rwanda

Rwanda imekuwa ikiendedesha harakati za upatanishi na pia kuwakumbuka waliokufa katika mauaji hayo


Mshukiwa wa mauaji ya kimbari nchini Rwanda Emmanuel Mbarushimana amekataa uendeshwaji wa kesi yake na mahakama ya Kigali kwa kutoa pingamizi kwamba hana haki zilizo sawa na mwendesha mashitaka.


Mshukiwa huyo alikabidhiwa Rwanda na nchi ya Denmark mapema mwezi wa saba mwaka huu ili kujibu mashitaka ya kuhusika katika mauaji ya kimbari ya mwaka 1994.


Mushukiwa huyo Bwana Emmanuel Mbarushimana amesema kesi yake haiwezi kusikizwa hadi pale atakapopata haki zilizo sawa na mwendesha mashitaka.


Hoja yake ilikuwa kwamba ni lazima na yeye aruhusiwe kukaa badala ya kusimama wakati kesi yake ikisikilizwa na wakati huo huo mwendesha mashitaka asimame badala ya kukaa kama ilivyozoeleka.


Aidha, amesema kuwa hajafurahia utaratibu unaotumiwa wa kuingia katika chumba cha mahakama ambapo mwendesha mashitaka na majaji wanaingia kwa kutumia mlango mmoja kinyume na mushitakiwa.


Mwendesha mashitaka amemshitaki kwa kushiriki katika mauaji dhidi ya watutsi yaliyotokea katika maeneo mbali mbali katika mkoa wa zamani wa Butare kusini mwa Rwanda.
Mushukiwa pia ameleta hoja nyingine ya kwamba hana wakili.
Swala hilo la kuwa na wakili lilikuwa limeshajadiliwa katika kikao cha kesi kilichotangulia ambapo alipewa muda wa kuchagua wakili anayetaka.


Wakati huo alipewa orodha ya mawakili 500 miongoni mwa mawakili wanaohudumu hapa nchini na kuikataa.
Alipendekeza kupewa orordha nzima ya mawakili wote kwa ujumla ili amchague mmoja anayetaka.Kipindi alichokuwa amepewa kuchagua wakili huyo kilikuwa kimemalizika.


Mahakama imesema kuwa hoja hizo haziwezi kuzuiya kesi hasa ikiwa ni kesi ya kukiri ama kukana mashtaka dhidi yake;jambo alilokataa kata kata akisema mahakama haina uhuru wala haki.


Imetangazwa kuwa Uamuzi kuhusu mabishano hayo utatolewa kesho.


Emanuel Mbarushimana mwenye umri wa miaka 50 alikabidhiwa Rwanda na mahakama ya Denmark mapema mwezi uliopita ili kujibu tuhuma za kuhusika kwake katika mauaji ya kimbari ya mwaka 1994.::
Chanzo Cha habari hii BBC SWAHILIHABARI  /  NA  AGAPE MSUMARI

MICHEZO || AJTC STARS KATIKA UZI MPYA PICHA KAMILI ZIKO HAPA

Chama cha waandishi  wa habari za michezo Tanzania kimetimiza ahadi yake ya kutoa jezi kwa chuo cha uandishi wa hababari na utangazaji arusha (AJTC) .
Ahadi hiyo  ni kufuatia ushindi walioupata katika bonanza la vyombo vya habari na utatangazaji  kanda ya kaskazini.





HABARI  NA PICHA  :: AGAPE MSUMARI

WANAFUNZI FUNGUENI BLOG

Nurdin Pallangyo (kulia)wa chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha alitoa maelezo juu ya wanafunzi wa AJTC kufungua blog kushoto ni mwandishi wa blog Udzungwa class Grace Frank.(Picha na Johaness Johnson)

NA.GRACE FRANK.
wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha wameshauriwa kufungua blog ili kuendeleza vipaji vyao.

MITINDO || TAZAMA PICHA ZA JINSI YAKUWEKA POZI TOFAUTI KWA KINA DADA WAKATI WAKUPIGA PICHA NZURI

 Kwa kina dada wale  ambao wanapenda kuonekana vizuri katika picha mbali mbali hii hapa ni muhimu kwao kujifunza namna yakukaa wakati unapiga pichazako 
                                                     TAZAMA PICHA HIZO HIZI HAPA








 HABARI NA JIMMY MINJA 

Tuesday, 12 August 2014

POLISI LIBYA AUAWA


HABARI NA GRACE FRANK.
Mkuu wa polisi katika mji mkuu wa Libya Tripoli, ameuawa na watu wasiojulikana.

TATIZO LA WANAFUNZI WA AJTC KUHAMA NA KWENDA KUPANGA


Mkufuzi wa chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha Adson Kagiye akihojiwa na mwandishi wa AJTC Radio Jesca Willy kuhusu wanafunzi wanaohama Hostel na kwenda kupanga vyumba.(Picha na Johaness Johnson)

HABARI NA JESCA WILLY

Wanafunzi  wa chuo cha uandishi wa habari na utangazaji  Arusha,  wanaoishi  nje  ya   hostel, wameshauriwa    kufuata  sheria  za  nchi, nakufuata  kilicho  weleta chuoni   hapo  ili  kutimiza  malengo  waliyo  jiwekea  katika  katika maisha yao.

HABARI KIMATAIFA || Polisi wa Misri watuhumiwa kwa mauaji


Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch, limesema kwamba vikosi vya askari wa Misri viliua idadi kubwa sana ya wananchi kuwahi kushuhudiwa ndani ya siku moja mwezi Agosti mwaka jana.

 Idadi hii inasemekana kuwa kubwa zaidi kuwahi kushuhudiwa duniani. Kwa muujibu wa taarifa zilizotolewa na kikundi hicho cha utetezi wa haki za binaadamu zinaeleza kwamba mauaji hayo ya waandamanaji waliokuwa wanampinga Raisi Mohammed Morsi,raia wapatao mia nane waliuawa katika uwanja wa Rab'a mjini Cairo mnamo tarehe 14 mwezi August mwaka 2013.

Kadhalika shirika hilo la kutetea haki za binadamu linasema kwamba mauaji hayo ya raia ni uvunjifu mkubwa wa haki za binadamu na kuwataka viongozi wenye dhamana wa Misri kutenda haki juu ya maisha ya raia hao.

Hayo yamesemwa na kiongozi wa shirika hilo, Kenneth Roth ambaye alizuiliwa kuingia ndani ya nchi ya Misri mapema wiki hii na kueleza alichokishuhudia na kuyafananisha na mauaji hayo na yale yaliyowahi kutokea katika uwanja wa Tiananmen nchini China.Chanzo BBC :: Habari Na Jimmy Minja 

UVIVU NI ADUI WA MAENDELEO

Fundi mitando bw.Aziz Mwinuka akitoa ufafanuzi juu ya mambo yanayoikabili studio za Ajtc Radio huku mwandishi wa Ajtc Bi.Lilian Deus( Picha na Nurdin Pallangyo)
Na.LILIAN DEUS.
Wanafunzi  wa  chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha (AJTC) wameaswa kutumi muda wao kufanya mazoezi kwa vitendo ya uandishi wa habari na kutangaza na kuandaa vipindi tofauti vya Radio ili wawaze kujijenga na kuwa wazuri katika tansia hii ya uandishi.

LIBERIA KUTUMIA ZMAPP KUTIBU EBOLA

Jopo la wataalam wa shirika la afya duniani WHO limeamua kwamba watu wanaweza kutumia dawa ambazo hazijajaribiwa katika mwili wa binaadamu kutibu ugonjwa wa ebola,iwapo maagizo fulani yataheshimiwa ikiwemo ruhusa ya mgonjwa.
Tangazo hilo linajiri huku shirika hilo likitangaza kuwa idadi ya watu waliofariki kutokana na ugonjwa huo imepita watu 1000 na kwamba kasisi wa uhispania aliyeondolewa nyumbani mwake baada ya kuambukizwa ugonjwa huo amefariki.
Kuidhinisha utumizi wa dawa ilio katika majaribio ni swala gumu.
Dawa hiyo ambayo haijajaribiwa imetumiwa na raia wawili wa kutoa msaada kutoka marekani ambao afya yao imeimarika,lakini kasisi huyo wa Uhispania ambaye pia aliitumia dawa hiyo ameaga dunia.
Watu wasiopungua 1,013 wameaga dunia kutokana na kuambukizwa virusi hivyo katika ukanda wa Afrika Magharibi.
Hatua hii ilichukuliwa huku Liberia ikitangaza kuwa ilihitaji kupata dawa la kufanyia majaribio liitwalo Zmapp baada ya kuiomba serikali ya Marekani.
Shirika la WHO lilisema kuwa lilikuwa limeombwa kupendekeza hatua hiyo kwa sababu ya kusambaa kwake na idadi kubwa ya vifo.

WHO imeruhusu dawa ya Zmapp kutumika kuzuia kuenea kwa Ebola
Shirika hilo lilisema kuwa mahali ambapo matibabu ya majaribio yanapofanyiwa panahitaji kuwa na ridhaa na matekeo ya jaribio hilo kukusanywa na kushiriki na wengine.
Katika ripoti iliyotolewa leo, shirika hilo linasema “Katika hali kama hizi za kuenea kwa ugonjwa huu, na iwapo masharti Fulani yataafikiwa, jopo hili limefikia makubaliano kuwa ni jambo la kimaadili kuingilia kati kwa mijarabu ambayo haijadhibitishwa huku ufanisi wake ukiwa haujulikani na adhari mbaya, kama matibabu au kinga.”
WHO ilitangaza kusambaa kwa ugonjwa wa Ebola kama janga la afya la dharura ulimwenguni.
Huku hayo yakijiri, serikari ya Liberia imesema kuwa madawa yatakayofanyiwa majaribio yatafikishwa nchini humo baadae juma hili – ingawa watengenezaji wa dawa madawa hayo Mapp Bio pharmaceutical walikuwa wameonya kuwa madawa hayo ni haba.
Zmapp imetumiwa kuwatibu wafanyikazi wawili wa US aid ambao walionyesha dalili ya kupata nafuu.

WHO imeruhusu dawa ya Zmapp kutumika kuzuia kuenea kwa Ebola nchini Liberia
Padri mmoja wa kanisa la Roman Catholic, aliyeambukizwa virusi vya Ebola nchini Liberia, na ambaye aliaga dunia baada ya kurejea nyumbani kwao nchuni Uhispania pia amedhaniwa kuwa alikuwa amepewa dawa hizo.
Hata hivyo, dawa hizo zimejaribiwa kwa nyani tu na bado haijatathminiwa kuwa ni salama kwa binadamu.
Shirika la afya dunini WHO linasema kuwa idadi ya watu waliokufa kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola magharibi mwa Africa sasa imepita watu 1000.
Hii leo wataalam hao wa WHO wamekubaliana kwamba utumizi wa dawa hizo utakubalika iwapo kutakuwa na uwazi huku rukhsa ikitolewa na wote wanaoshiriki katika tiba hiyo mbali na kuficha siri ya mgonjwa aliyetibiwa.

Na huku hayo yakijiri Liberia ambalo ndio taifa lililoathiriwa sana na ugonjwa huo lilianza kutumia dawa hizo kutoka marekani kabla ya uamuzi wa utumizi wake kutolewa na WHO.CHANZO NI BBC.HABARI NA JESCA WILLY

MADAKTARI WAUNDA MASIKIO TOKA UBAVUNI MWA KIJANA MWENYE MIAKA 9

HABARI NA LILIAN DEUS
Madaktari nchini Uingereza wameumba masikio kutokana na ubavu wa kijana aliyezaliwa bila ya viungo hivyo muhimu.

POLISI WA MISRI WAINGIA KATIKA TUHUMA ZA MAUAJI


Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch, limesema kwamba vikosi vya askari wa Misri viliua idadi kubwa sana ya wananchi kuwahi kushuhudiwa ndani ya siku moja mwezi Agosti mwaka jana.

WANAFUNZI WA AJTC WAASWA KUWA NA NIDHAMU WAKATI WA MITIHANI


Mwandishi wa Blog hii Aziz Mwinuka alifanya mahojiano na mmoja wa wanafunzi wa darasa la mount Udzungwa Nurdin Pallangyo kabla kuingia katika chumba cha mtihani.(Picha na Rajab Sultan)

ROUHANI: IRAN INA AZMA KATIKA MAZUNGUMZO YA NYUKLIA


 NA GRACE MBOYA
Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, Tehran ina azma thabiti katika mazungumzo ya nyuklia na kwa msingi huo ametoa wito kwa jamii ya kimataifa kutumia fursa iliyojitokeza kufikia mapatano kuhusu kadhia hiyo.

MAZINGIRA MACHAFU KERO KWA WAKAZI WA OLASIT.



















Twaha Yahaya mkazi wa Olasit akitupa taka katika eneo la barabara iliyopo karibu na makazi ya watu.(Picha na Grace Mboya.)


NA;
       Grace Mboya,
             ARUSHA.


 Wananchi wa kata ya olasiti iliyopo Mkoani Arusha wameulalamikia uongozi wa vijiji vyake kwa kutokuweka utaratibu mzuri wa utunzaji wa mazingira.

Waziri Mkuu Irak ahimizwa kuunda serikali

Waziri Mkuu mpya wa Irak, Haider al-Abadi
Waziri Mkuu mpya wa Irak, Haider al-Abadi

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon ameunga mkono uteuzi wa waziri mkuu mpya wa Irak, na kuonya kwamba mvutano wa kisiasa unaondelea nchini humo unaweza kuiingiza nchi hiyo katika mzozo mpana zaidi.

WANACHI WA KWA MOROMBO WAPO HATARNI KUPATWA NA MAGONJWA YA MILIPUKO


 Hili ni moja ya dimbwi lililopo katika makaazi ya watu lenye maji machafu (Picha na Charles Chami)

Wananchi wa eneo la kwa morombo mkoani arusha wapo hatarini kupatwa na magonjwa ya milipuko kutokana na uchafu wa mazingira katika maeneo hayo

Wednesday, 6 August 2014

MSICHANA ALIEPIGWA NA MTOTO WA OBAMA ATOA KAULI YA KUSHANGAZA





 

NA GRACE MBOYA
  Mtoto wa rais wa kike wa Marekani, Malia Obama mwenye umri wa miaka 16 alimpiga
/alimgonga