Chuo cha
uandishi wa habari na utangazaji cha jijini Arusha kimetangaza rasmi mashindano
ya utangazaji kwa wanafunzi wote chuoni hapo.
Akitoa taarifa
hiyo mkuu wa idara ya utangazaji kwa wanafunzi hao bwana onesmo mbise alisema
mshindi wa mwaka huu atazawadiwa kombe na fedha taslim shilingi elf 60, wakati
mshindi wa pili atapata shilingi elf 50 na mshindi wa tatu atajinyakulia kreti
mbili za soda.
Aidha bwana
mbise aliwataka wanafunzi hao kutumia muda uliobakia kujiandaa vilivyo na
mashindano hayo
Mashindano hayo
yanatarajiwa kufanyika kwa wiki moja kuanzia tarehe 21 mpaka 25 julai.
HABARI NA
AGAPE MSUMARI.

No comments:
Post a Comment